NAIBU MSEMAJI WA SERIKALI KUU MWANAISHA CHIDZUGA ATOA WITO KWA WAKENYA KUUNGA MKONO MRADI WA NYUMBA ZA BEI NAFUU.
Naibu msemaji wa serikali kuu Mwanaisha Chidzuga, ametetea mradi wa ujenzi wa nyumba za bei nafuu nchini, akisema kuwa umesaidia pakubwa wakenya wengi kupata nafasi za ajira. Chidzuga amesema kuwa zaidi ya vijana laki, mbili wamepata nafasi za ajira kando na akina mama wafanyabiashara, ambao huuza bidhaa za vyakula kwa wale wanaofanya kazi kwenye mradi […]



