ALIYEKUWA GAVANA WA KAUNTI YA MERU KAWIRA MWANGAZA AONA GIZA HUKU NAIBU WAKE ISAAC MUTUMA AKICHUKUA NAFASI YAKE RASMI.
Siku chache baada ya mahakama kutangaza kuwa bunge la seneti lilifuata utaratibu hitajika, katika mchakato wa kumbandua aliyekuwa gavana wa Meru, Kawira Mwangaza aliyekuwa naibu wake Isaac Mutuma sasa ameapishwa rasmi. Akizungumza mda mfupi baada ya kuapishwa, gavana Mutuma ameahidi kushirikiana na viongozi pamoja na wananchi wa matabaka mbali mbali katika kufanikisha shughuli za maendeleo […]



