Ratiba ya ligi kuu nchini Uingereza imetangazwa rasmi hii leo huku msimu mpya wa mwaka 2024/2025 ukitarajiwa kuanza rasmi tarehe 16 mwezi Agosti ambapo mechi ya kwanza itachezwa.
Mechi ya kwanza kabisa ya EPL msimu ujao ni ile ya Manchester United dhidi ya Fulham katika uwanja wa Old Trafford.
Hayo yanajiri huku matayarisho ya msimu mpya yakiendelea matarajio yakiwa mfumo wa uamuzi wa teknolojia ya VAR utaendelea kutumika hadi msimu ujao baada ya kura kupigwa majuma kadhaa yaliopita ambapo vilabu 19 vilipiga kura VAR iendelee kuwepo huku klabu moja pekee Wolveshampton ikipinga.

