MASHABIKI WA YOUNG BULLS NA SS ASSAD WALALAMA

Mashabiki wa klabu ya Young Bulls wanazidi kueleza kutoridhishwa na matokeo mazuri baada ya jana timu yao kupigwa mabao 5-1 dhidi ya Bumbani Stars nyumbani Alaskan.

Katika mechi ya jana mashabiki walianza kuondoka uwanjani mechi ikiendelea wakidai kuwa matokeo mabaya ya timu hiyo hayawavutii

Licha ya matokeo hayo mashabiki wengi walijitokeza jana wakiwemo viongozi wa kisiasa wa kaunti ya Kilifi. Meneja wa Young Bulls amethibitisha kuwa jana Young Bulls ilikusanya zaidi elfu 15k kama kiingilio pekee

Mashabiki wa klabu ya SS Assad kule Kwale wanasbinikiza klabu hiyo kufanya usajili katika dirisha dogo ili kuimarisha kikosi kipindi hiki ambacho timu inaandikisha matokeo mabaya

Taarifa zasema kuwa wikendi hii uhaba wa wachezaji ulionekana Bayana pale wachezaji 11 pekee na mmoja wa akiba ndio walisafiri kwenda Kisumu kuvaana na Vihiga United

Baadhi ya wachezaji waliachana na timu hiyo kutokana na mikataba yao kutoheshimiwa ambao ni pamoja na Feyswal Dzuya ambaye kwa sasa yuko kwao Mjanaheri eneo bunge la Magarini.