Beki wa Bayer Leverkusen, Jonathan Tah, yuko karibu kujiunga na Bayern Munich, Tah akitarajiwa kuwa mchezaji huru kuanzia tarehe mosi Julai 1, lakini mazungumzo bado yanaendelea kuhusu ada ya uhamisho, kwani Bayern wanamtaka awepo kwa ajili ya Kombe la Dunia la vilabu.
Iwapo makubaliano yatatimia, Tah anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya wiki hii, na Kusaini mkataba wa miaka minne.
Mapema mwezi huu Manchester United walikuwa na nia ya kumsajili, Barcelona Wakijitahidi kumsajili pia laikini pindi tu Bayern walipoingia katika kinyang’anyiro hicho, uamuzi wa Tah ulikuwa tayari umefanyika.

