INTER MILAN WASHINDA UBINGWA ITALIA

Klabu ya Inter Milan Kule Italia ndio mabingwa wa kombe la Coppa Italia baada ya kukaranga Fiorentina kichapo cha mabao 2-1 katika fainali iliyochezwa katika dimba la Stadio Olimpico uwanja ulioko Roma.

Mabao mawili la mshindi wa kombe la dunia Lautaro Martinez raia wa Argentina aliyofunga katika dakika ya 29 na 37 ndio yaliyotosha kuishindia Inter Milan ubingwa wao wa tisa wa kombe hilo.

Rafiki ikumbukwe kwamba miamba hao wa Milan watakuwa wanavaana na Manchester City katika fainali za Uefa tarehe 10/06 mwaka huu.