Klabu ya Young Bulls imesajili ushindi wa bao 1-0 dhidi ya klabu ya Rainbow fc katika uwanja wa shule ya upili ya malindi kaunti ya Kilifi.
Bao la ushindi na lakipekee katika mechi hiyo limefunga na Alex Mwalimu na kuwafanya vijana hao wa mkufunzi Ali Said Gaucho kurefusha pengo lao na nafasi ya pili hadi alama 9.
Kwa sasa klabu ya Young Bulls inaongoza ligi hiyo wakiwa na alama 39 na mkurugenzi mkuu wa klabu hiyo Johnson Mwabati anasema lengo lao kubwa msimu huu ni kusajili matokeo mazuri katika mzunguko wa pili wa ligi na kupanda hadi ligi ya National Super League.
Mwabati ameambia Tama La Spoti kwamba licha ya kuwepo kwa tetesi nyingi za uhamisho dirisha la uhamisho litakapofunguliwa rasmi, klabu hiyo itasajili wachezaji wenye tajriba pekee ili kusaidia klabu hiyo kupata kasi hadi kupanda daraja.
Rafiki Young Bulls mpaka kufikia sasa bado haijapoteza mechi hata moja kwenye ligi ya daraja la kwanza.

