Ipo haja ya sheria za fkf pamoja na zile za katiba ya kenya kufanyiwa ukarabati ili kuwiana kwenye masuala ya uendeshaji wa soka la Kenya iwapo taifa hili lingesonga mbele kimichezo.
Ni kauli ya mgombea wa urais wa fkf nchini Tom Alila katika mdahalo ulofanyika katika mgahawa mmoja jijini Nairobi ambapo wagombea walipewa fursa ya kunadi mipango yao iwapo watachaguliwa kwenye ofisi za shirikisho.
Kulingana na Alila ni kuwa makuzi ya soka yanafaa kuanzia shuleni na mashinani zaidi kwani mara nyingi wanafunzi huwa shuleni tofauti na nyumbani na hapo ndio rahisi kulea talanta za wachezaji hao.
Vilevile Alila anasema ipo haja ya sheria za fkf kubadilisha kipengele cha idadi ya wapiga kura kwani wachezaji wengi nchini wanahisi kufungiwa kwenye kuchagua viongozi wao kutokana na sheria inayoruhusu idadi chache pekee kupiga kura
Uchaguzi mkuu wa fkf wa kitaifa unatarajiwa kufanyika tarehe 7 mwezi Disemba mwaka huu.

