Mkufunzi wa klabu ya Sango Sportiff inayoshiriki ligi ya Divisheni ya Pili Coach Rigo, ameelezea kwamba kurekebisha makaosa waliyofanya kwenye mechi yao Iliyopita, Ndio Kulichangia Ushindi wao Mnono Dhidi ya Mariakani Fc, akiusifia Mchezo Mzuri ulioonyeshwa na Upande huo wa Mkufunzi Hassan Seif.
Sportiff waliicharaza Mariakani magoli Manne bila jawabu kwao nyumbani, Timu Hio sasa Ikishikilia nafasi ya Pili na alama Ishirini na Tisa baada ya Mechi Kumi ni Mbili, Kukiwa na Utofauti wa mechi nne na alama tisa Kati yao na vinara wa Ligi Simba Apparel.
Aidha Coach Rigo ameongezea kwa Kusema Ya kwamba wanajitayarisha Vilivyo Kuwakabili Sparki Youth, azimio Lao Likiwa Lilee la kuvuna Alama Tatu, mechi Hio ikiratibiwa Kupigwa Siku ya Jumapili tarehe mbili ugani Santiago Itsowe.

