MWENDWA ANAIMANI NA SOKA LA KINADADA

Rais wa shirikisho la soka hapa nchini Kenya FKF amethibitisha kuwa soka la kinadada sio Kenya pekee bali kimataifa ndio soka ambalo kwa siku za hivi karibuni linakua kwa kasi sana.

Amesema kwa sasa kama shirikisho, FKF wameanza kupanga mikakati ya kuimarisha hata zaidi soka la kinadada ili kuenda na wakati jinsi ulimwengu unavyofanya kwa sasa pamoja na kuhakikisha soka lao linafuata sheria zote za soka.

”Sasa kila mtu anaona kwamba soka la kinadada limeanza kukua, hapa Kenya tumeanza mpango wa kuimarisha soka la kinadada. Tunataka pia soka la kenya lianze kufuata mkondo wa kuzingatia sheria za kimataifa.” Alisema Mwendwa.

Pia mwendwa ameonyesha matumaini ya kukua kwa soka la Kenya kwa jumla akizungumzia jinsi viwanja vimeanza kuboreshwa na tukio la wachezaji wa Kenya kuanza kuuzwa kwa vilabu vya kimataifa jambo ambalo lilikuwa kwa uchache miaka ilopita.

”Kenya tumeanza kukua, kwa sasa tumeanza kuuza wachezaji katika vilabu vya matifa ya kigeni.” Aliongeza Mwendwa