MESSI AWEKA REKODI

Lionel Messi sasa ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza katika historia ambaye ni mshindi wa kombe la dunia kufikisha mabao zaidi ya mia moja katika mechi za kimataifa.

Messi alifanya hivyo jana baada ya kufunga hatrick ndani ya kipindi cha dakika 36 katika mechi ambayo mshambuliaji huyo aliisaidia timu yake ya Argentina kushinda kwa mabao 7-0.

Leonel Messi sasa amefikisha jumla ya mabao na assist 28 katika mechi 14 za hivi punde zaidi alizochezea timu ya Argentina.