MECHI MBILI KUBWA ZA UEFA KURINDIMWA USIKU WA LEO

Mashindano ya klabu bingwa ulaya hatua ya 16 bora yatakuwa yanarejea usiku wa leo na mechi mbili zimeratibiwa kurindimwa.

Vijana wa mkufunzi Antonio Conte Tottenham Hotspurs usiku wa leo watakuwa wanasafiri kukipiga dhidi ya mabingwa mara saba wa klabu bingwa Ulaya Ac Milan katika dimba la San Siro.

Katika dimba lengine leo ni kwamba Parc de Princess kutashuhudiwa ngarambe nzito kwelikweli wakati ambapo PSG watakuwa wanavaana na miamba wa ujerumani Bayern Munich, mechi ambayo itakuwa inachezwa mwendo wa saa tano usiku.