MANCHESTER UNITED YATHABARUKU UBINGWA

Klabu ya Manchester united jana ilisajili ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Newcastle united katika mtanangwe wa fainali za Carabao uliochezwa katika uwanja wa wembley.

Bao la kiungo Casemiro pamoja na lile la Marcus Rashford ndiyo mabao yalotosha kuwapa ushindi vijana hao wanaoongozwa na mkufunzi Erik Ten Hag.

Kombe la Carabao waloshinda Manchester United jana chini ya uongozi wa mkufunzi mpya ndio kombe la kwanza kushinda tangu mwaka 2017 chini ya mkufunzi Jose Mourinho.