Shirikisho la soka duniani Fifa limetangaza kwamba sasa marefa watakuwa wanatangaza moja kwa moja matokeo ya maamuzi ya VAR kwa mashabiki uwanjani.
Kulingana na rais wa fifa Gianni Infantino ni kwamba utaratibu utasaidia kupunguza taharuki inayotokana na mashabiki kutoelewa maamuzi ya refa uwanjani na sasa mawasiliano yanafaa kufanyika parawanja.
Ni hatua ambayo awali ilikuwa imeungwa mkono na wadau wa soka ulaya na utaratibu huo utaanza rasmi katika mashindano ya Fifa Club World Cup yatakayofanyika nchini Morocco.

