Mabingwa wa ligi kuu nchini Kenya mwaka 2008 Mathare United wamethibitisha kumwajiri Boniface omondi kama mkufunzi wao kwa kipindi cha mwaka mmoja.
Omondi sasa anaungana na klabu hiyo ya mitaa ya mabanda jijini Nairobi baada ya kukiongoza kikosi cha vijana wachanga wa kariobangi sharks kwa kipindi cha miaka mitano.
Mathare United walikosa mechi tatu za mwanzo wa msimu huu kutokana na kesi iliyokuwa inasubiri maamuzi kutoka kwa kamati ya kusuluhisha migogoro ya michezo ambayo iliamua kwamba Mathare watasalia kwenye ligi licha ya kamati ya mpito msimu ulopita kuishusha daraja.

