Mkufunzi mkuu wa klabu ya Barcelona Xavi Hernandez amepongeza wachezaji wake kwa ushindi wa 3-2 wa timu yake ugenini dhidi ya Paris Saint-Germain katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa robo fainali ya klabu bingwa barani Ulaya, akisisitiza kwamba ilionyesha Wakatalunya hao wanaweza kwa mara nyingine tena kushindana na timu bora zaidi barani Ulaya.
Barcelona wanaonekana katika hatua ya nane bora ya Ligi ya Mabingwa kwa mara ya kwanza tangu 2020, walipofungwa 8-2 na Bayern Munich mjini Lisbon, na tangu Lionel Messi aondoke kwenye klabu hiyo.
Kocha huyo anatazamia mechi ya mkondo wa pili ya kusisimua zaidi. Huo ulikuwa ushindi wao wa kwanza ugenini katika awamu ya muondoano ya shindano hilo tangu 2019.

