KAUNTI YA KILIFI KUAJIRI WACHEZAJI WANAOWAKILISHA KAUNTI KWENYE MICHEZO YA KYISA

 

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gideon Maitha Mung’aro ameahidi kuwaangalilia nafasi za ajira baadhi ya vijana wanaoshiriki mashindano ya KYISA kaunti ya Tharaka Nithi endapo wataishindia ubingwa kaunti ya Kilifi kwenye ngarambe hizo.

Haya ni kulingana na Waziri wa Michezo kaunti ya KILIFI Daktari Dama Masha,akisema wameweka kigezo hicho ili kuwapa motisha zaidi ya kufanya vyema.

Akizungumza huko Tharaka Nithi,Dama amesema Kilifi inawakilisha eneo zima la Pwani kwa kuwa ndiyo kaunti pekee ya Pwani inayoshiriki makala hayo ya nane.

Hata hivyo ameelezea matumaini yake kwamba kikosi hicho kina uwezo  wa kufanya vyema.