Wadau mbalimbali wa elimu katika kaunti ya Taita Taveta wameanzisha mafunzo kwa wanafunzi wa shule za upili kuhusu suala la maadili na namna ya kujiepusha na visa vya ufisadi.
Mmoja wa wadau hao Shadrack Mutungi amesema wanashirikiana na maafisa wa tume ya maadili na kukabiliana na ufisadi kwenye mafunzo hayo na kuitaja kama hatua ambayo itasadia kwa asilimia kubwa kuwalinda wanafunzi dhidi ya kujihusisha na visa vya ufisadi baada ya kumaliza masomo yao.
Aidha, amesema kuna hatua ambazo zimepigwa katika kukabiliana na visa vya ufisadi kaunti ya Taita Taveta.
WADAU KWENYE SEKTA YA ELIMU KAUNTI YA TAITA TAVETA WAANZISHA MAFUNZO KWA WANAFUNZI WA SHULE ZA UPILI

