BENJAMIN DALU TAYARI ATEULIWA KUWA MWENYEKITI WA BODI YA KPA

Aliyekuwa mbunge wa eneo bunge la Kinango kaunti ya Kwale Benjamin Dalu Tayari ameteuliwa kuwa mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa mamlaka ya bandarini nchini KPA.

Katika taarifa kwenye gazeti rasmi la serikali waziri wa barabara na uchukuzi nchini Kipchumba Murkomen amemteua Benjamini Dalu Tayari kwenye wadhifa huo kwa muda wa miaka 3.

Anachukua wadhifa huo kutoka kwa mtangulizi wake Joseph Kibwana huku mchakato wa kumtafuta mkurugenzi mkuu mpya kwenye mamlaka hiyo ya KPA ukiendelezwa.