Huenda matatizo ya uhaba wa maji katika eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi yakapata suluhu la kudumu.
Hii ni baada ya wizara ya maji katika kaunti Kilifi kutekeleza zoezi la kutathmini chanzo cha tatizo hilo na jinsi linaweza kutetuliwa kwa haraka na kuongeza kuwa watatoa ripoti kamili kuhusiana na zoezi hilo hivi karibuni.
Kwa mujibu wa waziri wa maji na mazingira katika kaunti hii ya kilifi, Omar Saidi ni kuwa wataaza kusambaza maji katika eneo bunge hilo la Magarini pamoja na kuchimba visima vya maji katika eneo hilo.
Kwa upande wao baadhi ya wakaazi wa eneo la Adu eneo bunge hilo la Magarini wameisisitiza serikali ya kaunti ya KIlifi kuchukulia kwa uzito suala la ukosefu wa maji katika eneo hilo la Adu.
TATIZO LA UHABA WA MAJI ENEO BUNGE LA MAGARINI KAUNTI YA KILIFI KUPATA SULUHU LA KUDUMU

