SERIKALI YA KAUNTI YA KILIFI YATEUA UPYA WAZIRI WA BARABARA.

Aliyekuwa afisaa mkuu wa barabara kaunti ya Kilifi, Philip Charo ametauliwa kuhudumu katika nafasi ya katibu wa serikali ya kaunti ya Kilifi na waziri wa barabara kaunti hii.

Uteuzi wa Charo, umefanyika baada ya aliyekuwa waziri wa barabara hapa kaunti ya Kilifi, Catherine Kenga, kuchaguliwa na wawakilishi wadi kaunti ya Kilifi, kuhudumu katika nafasi ya spika wa bunge la kaunti.

Akitoa taarifa hiyo, msemaji wa serikali ya kaunti ya Kilifi, Jonathan Mativo, amesema Hezekaih Mwarua, pia amekabidhiwa nafasi ya afisa mkuu katika afisi ya gavana wa kaunti ya Kilifi, Gideon Maitha Mung’aro.

Aidha, ameelezea kuwa hatua hii ni kuhakikisha kuwa shughuli za serikali ya kaunti ya Kilifi, zinaendelezwa kama kawaida.