KOCHA WA BUMBANI STARS AIGURA KLABU HIYO

Kocha Mwaduka Bakari ambaye aliipandisha klabu ya Bumbani Stars kutoka Lungalunga ligi ya daraja la kwanza kitaifa msimu uliopita amethibitisha kuwa amefanya maamuzi na sasa ameachana na klabu hiyo.

Kocha huyo ametaja kukosewa heshima na uongozi miongoni mwa masuala mengine yaliyojiri punde tu baada ya msimu jana kutamatika mambo ambayo amekiri yalimfanya kuhisi kujikataa klabuni hapo.

Mwaduka ambaye ni mmiliki wa cheti cha ukocha cha CAF C amethibitishia Tama La Spoti kuwa kwa sasa yupo nyumbani ila klabu ambayo itahitaji huduma zake yupo tayari kwa mazungumzo