Gavana wa kaunti ya Mombasa Abdulswamad Shariff Nassir, anapanga kufanya ukaguzi ili kubaini wafanyikazi halali walioajiriwa na serikali ya kaunti ya Mombasa.
Akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa maabara ya kidijitali ya BIONEAR, katika ukumbi wa Treasury Square kaunti ya Mombasa, Nassir amesema kuna baadhi wafanyikazi hewa ambao wanalipwa mshahara kila mwezi na serikali ya kaunti hiyo.
Nassir amesema hatua hiyo itasaidia pakubwa kutambua ni nani anayestahili kulipwa mshahara na serikali ya Mombasa, kwani imekuwa ikipoteza mabilioni ya pesa kulipa wafanyikazi hewa.
Maabara hayo ya BIONEAR, yatasaidia kupeleka huduma ya afya kwa jamii maeneo ya mashinani na hata kuboresha sekta ya afya Mombasa.
Miongoni mwa vipimo vitakavyotolewa maabara hiyo cha Covid-19, Ukimwi, Kifua kikuu (TB) miongoni mwa vipimo vingine..
GAVANA ABDULSWAMAD SHARIF NASSIR APANIA KUFANYA UKAGUZI KUBAINI WAFANYIKAZI HEWA MOMBASA

