WAKENYA WOTE NCHINI WAAHIDIWA KUPATA MIRADI YA MAENDELEO.

Mkuu wa watumishi wa umma nchini Felix Koskei amesema kuwa serikali ya kitaifa haijatenga eneo lolote kimaendeleo katika taifa hili.

Koskei amesema kuwa sharti wakenya wa maeneo yote humu nchini wanufaike na miradi ya maendeleo, ikatoyoboresha maisha mashinani.

Akizungumza katika kaunti ya Marsabit, Felix amesema kuwa tayari wanakandarasi, wamerejeshwa katika maeneeo tofauti ya taifa hili, kukamilisha miradi iliyokwama kwenye serikali ya awali.

Koskei amesema kuwa wanashirikiana na viongozi wa bunge la kitaifa, katika kuhakikisha kuwa miradi hiyo inakamilishwa kwa mda unaostahili.