WAKENYA WAONYWA DHIDI YA USAMBAZAJI WA TAARIFA GUSHI MITANDAONI.

Taifa la Kenya linakabiliwa na changamoto kuu ya uenezaji wa taarifa za uongo kupitia mitandao ya kijamii.

Haya ni kwa mujibu wa msemaji wa serikali Isaac Mwaura ambaye amesema kuwa, asilimia hamsini ya wakenya wamekuwa wakihadaiwa kupitia mitandao jambo ambalo limechangia kuchipuka kwa tofauti kati ya wakenya na serikali inayo waongoza.

Akizungumza katika kikao na waandishi wa habari, Mwaura amesema hatua hiyo imesababishia serikali changamoto kuu katika kuwaeleza wakenya ukweli kuhusiana na masuala mbali mbali katika uongozi wake.

Wakati uo huo Mwaura amewataka wakenya kuwa wazalendo na kusitisha masuala ya kukandamiza utendakazi wa serikali kupitia uenezaji wa taarifa ghushi mitandaoni.