Klabu ya Malindi Young Bulls sasa wamepoteza mechi yao ya kwanza ya daraja la kwanza kitaifa baada ya kutandikwa na Dandora Youth kichapo cha bao 1-0 katika dimba la Komarock jijini Nairobi.
Wakati hayo yakijiri wenzao wa Malindi Progressive academy jana katika uwanja wa Alaskan walisajili ushiondi wa mabao 3-1 dhidi ya wanajeshi wa Kenya navy. 3K FC walipiga sare ya bao 1-1 dhidi ya klabu ya Ruiru Hotsters wakati Buruburu pia walilazimishwa sare ya 1-1 katika uwanja wao wa nyumbani na Vapour Sports.
Gor mahia Youth ilipigwa mabao 2-0 dhidi ya Kibera Soccer na hatimaye wanabenki Equity waliindanika Balaji EPZ kichapo chja bao 1-0.
Katika mechi za daraja la pili kitaifa ni kwamba viongozi wa ligi Omax FC inayoongozwa na mkufunzi Juma Kalato ilisajili ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Sparki Youth katika uwanja wao wa nyumbani.
Simba Apparel walishinda Samburu Lions kwa kichapo cha 1-0 na hatimaye Kishada katika uwanja wao wa nyumbani wakipigwa na Deep Sea inayoongozwa na mkufunzi Athman Pirezi kichapo cha bao 1-0.

