Klabu ya Manchester United sasa imetinga fainali za kombe la Carabao baada ya kuitandika Nottingham Forest kichapo cha mabao 2-0 kwenye mechi ya marudiano ya Semi Fainali, mtanange uliochezwa katika dimba la Old Trafford usiku wa kuamkia leo.
Bao la fowadi wa timu ya taifa ya Ufaransa Antony Matial pamoja na lile la kiungo wa Brazil Fred ndio yaliyotosha kuwapa ushindi vijana hao wa mkufunzi Erik Ten Hag.
Manchester united sasa itakutana na Newcastle United katika fainali itakayochezwa tarehe 26 mwezi huu wa Febraury katika uwanja wa Wembly Uingereza.

