Mwenyekiti wa muungano wa madalali wa bima AIBK, Antony Mwangi amesisitiza haja ya mtaala wa elimu wa umilisi CBC nchini kuidhinisha somo la bima kwenye shule za msingi hadi vyuo vikuu.
Mwangi amesema kuwa hatua hiyo itawezesha wanafunzi kujua na kuelewa umuhimu wa bima maishani.
Mwangi ameyasema haya katika kongamano la 16 eneo la diani kaunti ya kwale kwenye kikao na waandishi wa habari.
Aidha mwenyekiti huyo amesema ni wakati sasa wa mshikamano kama kampuni za bima ili kukabiliana na ushindani wa biashara za kimataifa.
MADALALI WA BIMA YA AIBK WATAKA MTAALA WA CBC KUIDHINISHA SOMO LA BIMA

