ST MARYS KITENDE WASHINDA SOKA LA AFRIKA MASHARIKI

St Marys Kitende ya Uganda sasa ndio mabingwa wa mashindano ya soka kwenye michezo ya shule za upili yanaoendelea nchini Tanzania Arusha baada ya kuitandika shule ya upili ya Ebwali inayotokea Kenya kichapo cha mabao 4-0.

Huu unakuwa ubingwa wa 12 kwa St Marys Kitende katika mashindano ya soka ya shule za upili za  Afrika Mashariki yalioanza mwaka wa 2002.