Gavana wa kaunti ya Taita Taveta Andrew Mwadime ametakiwa kuhakikisha kuwa anakamilisha miradi ya maendeleo ambayo haikukamilika wakati wa gavana aliyeondoka Granton Samboja.
Wanaharakati wa kijamii wakiongozwa na Juma Kombora wametoa shinikizo hizo kwa gavana Mwadime wakisema kuwa miradi hiyo ilipania kuwanufaisha wananchi hivyo ni sharti imalizwe.
Kombora amesema kuwa miradi hiyo pia inapaswa kutengewa fedha za kutosha ili ikamilike kwa wakati ufaao.
Wakati huohuo amesisitiza haja ya afisi ya gavana na bunge la kaunti kushirikiana kwa minajili ya kupitisha miswada ambayo ilikwama hususan ile ambayo ingewanufaisha wakaazi wa kaunti hiyo.
GAVANA ANDREW MWADIME ATAKIWA KUKAMILISHA MIRADI YA MAENDELEO AMBAYO HAIKUMALIZWA NA MTANGULIZI WAKE

