ZIWA KENYATTA KAUNTI YA LAMU YAENDELEA KUKAUKA

Ukame pamoja na uvamizi wa ardhi kando kando ya Ziwa Kenyatta eneo la Mpeketoni kaunti ya Lamu umesababisha ziwa hilo kuendelea kukauka.
Kwa mujibu wa serikali ya kaunti ya lamu, Asilimia 75 ya Ziwa Kenyatta imekauka kutokana na shughuli mbalimbali zinazoendelea kufanyika karibu na ziwa hilo.
Ziwa hilo hutegemea maji ya Mvua yanayopitia mikondo ya maji inayoanzia maeneo ya Msitu wa Boni kuelekea Widhu, Pangani, Lumshu na Mugumoini.
Kulingana na mwenyekiti wa ufuo wa Ziwa Kenyatta Samwel Musyoka pamoja na gavana wa kaunti hiyo Issa Abdalla Timamy Ziwa Kenyatta hutegemewa sana na wakazi wa Mpeketoni pamoja na mifugo wao Lakini sasa hakuna mvua.