Viongozi wa kidini katika kaunti ya Lamu wameshinikiza serikali ya kitaifa kushukisha gharama ya bei ya chakula hasa bei ya unga wa ugali ili wanachi wapate afueni .
Wakizungumza wakiwa Mpeketoni wamesema ugali ni chakula kinacholiwa na idadi kubwa ya wananchi na kwamba kwa sasa wengi wamekosa chakula majumbani kutokana na bei ya juu ya bidhaa hiyo.
Kulingana na Viongozi hao itakuwa vyema iwapo Rais William Samoei Ruto atatimiza ahadi alizoahidi wakati wa kampeni zake za uchaguzi.
Vilevile, wamesema kutokana na hali ya kupanda kwa gharama ya maisha vijana wengi sasa wanajihusisha na visa vya uhalifu na utumizi wa dawa za kuleva.
VIONGOZI WA KIDINI KAUNTI YA LAMU WAITAKA SERIKALI KUSHUGHULIKIA GHARAMA YA JUU YA MAISHA

