MKUFUNZI wa zamani wa klabu ya Manchester City, Sven-Göran Eriksson, raia wa Sweden, aaga dunia akiwa na umri wa miaka 76.
Hadi anaaga dunia, Sven alikuwa amenoa vilabu vya soka 13 na timu 3 za taifa ikiwa ni pamoja na timu ya taifa ya Uingereza, THE THREE LIONS, kati ya mwaka 2001 hadi 2006.
Vilabu maarufu alivyowahi kuvipatisha makali ni pamoja na Manchester City, Leicester City, Roma, Benfica, Sampdoria na Lazio.
Ivory Coast au Côte d’Ivoire kama inavyotambulika na FIFA ni timu ya pekee kutoka Afrika kuwahi kunolewa na Sven. Sven aliwasaidia NDOVU hao kufuzu kucheza kombe la dunia 2010.
Wakati anateuliwa kuwa meneja wa Uingereza Sven Goran Eriksson aliingia kwenye vitabu vya kumbukumbu kama meneja wa kwanza wa kigeni nchini humo kukinoa kikosi cha Uingereza.
Sven alikuwa maarufu sana nchini Uingereza, hata ulihitaji tu kutaja jina lake la kwanza na kila mtu – awe ni shabiki wa soka au la – alijua unazungumza nani.
Sad to hear about the passing of Sven-Göran Eriksson. I met him several times as England manager and was always struck by his charisma and passion for the game. My thoughts are with his family and friends. A true gentleman of the game. W
— The Prince and Princess of Wales (@KensingtonRoyal) August 26, 2024
“Kwa niaba ya jumuiya ya soka la Ulaya, kila mtu UEFA amehuzunishwa sana na kifo cha Sven Göran Eriksson,” UEFA imesema katika mtandao wa X zamani ukijulikana kama Twitter.
“Akiwa mpendwa kwenye mchezo huu wa soka, Sven alikuwa mshindi wa Kombe la UEFA kama kocha wa IFK Göteborg mnamo 1982 kabla ya kuiongoza Lazio kwenye ushindi wa Kombe la UEFA mnamo 1999.”
On behalf of the European football community, everybody at UEFA is deeply saddened to learn of the passing of Sven Göran Eriksson.
A beloved figure in the game, Sven was a UEFA Cup winner as coach of IFK Göteborg in 1982 before leading Lazio to the UEFA Cup Winners’ Cup in 1999.… pic.twitter.com/ZlNSFftl97
— UEFA (@UEFA) August 26, 2024

Klabu ya Liverpool na Fiorentina ni baadhi ya vilabu ambavyo tayari vimetoa rambirambi kuomboleza kifo cha nguli huyo wa soka.
“Pumzika kwa amani, Sven-Göran Eriksson. Mawazo ya kila mtu kwenye klabu yako pamoja na familia na marafiki wa Sven katika wakati huu wa huzuni sana,” Liverpool imeandika kwenye mtandao wa X.
Rest in peace, Sven-Göran Eriksson.
The thoughts of everyone at the club are with Sven’s family and friends at this extremely sad time. pic.twitter.com/vn5qkn5RWc
— Liverpool FC (@LFC) August 26, 2024
Man City wameandika kwenye X wakisema, “Tungependa kutoa rambirambi zetu za dhati kwa familia na marafiki wa Sven-Goran Eriksson, ambaye ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 76. Pumzika kwa amani, Sven.”
We would like to express our sincere condolences to the family and friends of Sven-Goran Eriksson, who has passed away at the age of 76.
Rest in peace, Sven. 🩵
— Manchester City (@ManCity) August 26, 2024
BURIANI SVEN.

