FRED MATIANG’I ASISITIZA WAKENYA KUDUMISHA AMANI.

Aliyekuwa waziri wa usalama nchini Dkrt Fred Matiang’I, amewaonya wakenya dhidi ya kuchochewa na wanasiasa kuendeleza hasama kati yao.

Kulingana na Matiang’I, wakenya wanapaswa kudumisha umoja na kuendelea kuwa na imani ya kubadilika kwa hali ngumu za kiuchumi, ambazo zimeendelea kukumba taifa hili kwa sasa.

Aidha, kiongozi huyo ambaye ametangaza nia yake ya kuwania urais mwaka 2027, amesisitiza haja ya umoja na amani kuendekezwa na wakenya wote katika taifa hili.

Kwa upande wake aliyekuwa naibu wa Rais, Rigathi Gachagwa amemuonya rais William Ruto, dhidi ya kutumia wandani wake kuendeleza kashfa dhidi ya rais mstaafu Uhuru Kenyatta.