Wandani wa rais William Ruto wamejitokeza kupongeza hatua ya wakenya wengi zaidi kujitokeza kwenye mikutano ya rais William Ruto, katika eneo la Mlima Kenya.
Wakiongozwa na kiongozi wa wengi kwenye bunge la Seneti, Aaron Cheriyot amemkashifu aliyekuwa naibu wa rais Rigathi Gachagwa, kwa madai ya kushawishi wananchi wa eneo hilo, kutojitokeza kwenye mikutano hiyo.
Kauli yake imepigwa jeki na Faruk Kibet, msaidizi wa rais William Ruto, anayesema kuwa hatua ya wakenya kujitokeza kwenye zaira ya rais eneo la mlima Kenya, kuna dhihirisha kuwa wamezika siasa za ukabila katika kaburi za sahau.
Faruk vile vile amemsuta Gachagwa, kwa kile alichosema hawezi kuongoza taifa iwapo ataendeleza siasa za ukabila.

