GAVANA ISSA TIMAMY NDIYE KAIMU KINARA WA CHAMA CHA ANC

Gavana wa kaunti ya Lamu Issa Abdalla Timamy Sasa ndiye kaimu kinara wa chama cha ANC.
Hii ni baada ya Kinara wa chama hicho Musalia Mudavadi kujiuzulu wadhifa huo kufuatia uteuzi wake kuwa waziri mkuu serikalini.
Hatua hiyo inaafiki matakwa ya kipengee cha 77(2) cha katiba kinachomzuia afisa wa serikali kuwa na ofisi ya chama cha kisiasa.
Kaimu kiongozi wa chama cha ANC aliteuliwa na baraza la ANC kwa mujibu wa katiba ya chama hicho.
Timamy amekuwa naibu mwenyekiti wa chama cha ANC kuanzia mwaka wa 2015 baada ya chama hicho kubuniwa rasmi na mnamo mwaka 2013 alichaguliwa kuwa gavana wa kaunti ya Lumu kupitia chama cha UDF.
Mwaka wa 2017 alitumia chama cha ANC kuwania wadhifa huo kwa mara ya pili na kushindwa kwenye kipute hicho na Fahim YassinTwaha wa Jubilee.
Mwaka huu wa 2022 Timamy aliwania tena wadhifa huo akitumia chama cha ANC kilichokuwa kwenye muungano wa Kenya Kwanza na kumbandua Fahim Yassin Twaha.