MAKABURI ZAIDI YATABULIWA KATIKA ENEO LA KWA BINZARO HAPA KAUNTI YA KILIFI.

Makaburi mengine saba, mafuvu, na mifupa ya binadamu  imepatikana  katika kijiji cha Kwa Binzaro  kaunti ya Kilifi .

Afisa mkuu wa upelelezi kaunti ya Kilifi Robert Kiinge, amethibitisha matukio hayo huku akihofia  kwamba huenda  wafuasi wengi wa dhehebu potofu wamefariki katika eneo hilo.

Kiinge amesema kuwa  makaburi hayo, niya  kina kifupi  mno  na waathiriwa walizikwa kwa kutumia makaratasi ya lailoni.

Vilevile kiinge amefichua kuwa shughuli ya ufukuzi wa makaburi hayo zitaanza hivi karibuni kama ilivyoagiza mahakama kuu ya Malindi.

Aidha, kiinge ameeleza hofu ya kuwa huenda watoto sita walioripotiwa kupotea kuwa ni miongoni mwa milli iliyozikwa eneo hilo.

Haya yanajiri huku watu 11 wakisalia korokoroni, wakati  uchunguzi unapoendelea.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *